Home
  • Mawasiliano
  • Mwanzo
  • Rozari hai
    • Dira ya Rozari Hai
    • Dhamira ya rozari hai
    • Mafundisho Rozari
    • Kuhusu Skapulari
    • Matokeo ya Bikira Maria
    • Nguvu ya rozari
    • Historia ya Rozari Takatifu
  • Novena
    • Novena za kila mwezi
  • Watakatifu
    • Kuhusu Mt. Philomena
    • Historia ya Mt.Filomena
    • Historia ya Mwenyeheri Paulina Mariae Jaricot
  • Sala na kazi
  • Matendo ya Huruma
  • Habari na Matukio
    • Habari
    • Picha
    • Matokeo ya Fatima
  • Makala
  • Wanachama
    • Uanachama
    • Wajibu wa Mwanachama
    • Michango ya Hiari
  • Uhamasishaji wa Rozari Hai
  • Wanafunzi wa St Martin Girls Secondary Morogoro wameanza kusali mafungu yao ya Rozari Hai 26 May 2022
  • Uhamasishaji Rozari Hai Iringa na kupokea wanachama wapya
  • Uhamasishaji Rozari Hai Canosa Girls na kupokea wanachama wapya

Historia ya Rozari

Rozari takatifu ni sala kutoka Mbinguni. Bikira Maria alimkabidhi Mtakatifu Dominiki mwaka 1214 katika msitu wa Toulouse ambapo alienda kwa mafungo. Huko alisali usiku na mchana bila kula wala kunywa akifanya toba na malipizi.

Usiku wa siku ya tatu alizimia ndipo Bikira Maria alimtokea akiwa amefuatana na malaika watatu na alimkabidhi Mtakatifu Dominiki Rozari Takatifu, kisha akamfundisha namna ya kuisali. Alimfundisha matendo ya furaha, uchungu na utukufu kwa maana ya kusali tasbihi tatu ambazo ni Rozari moja. Papa Yohane Paulo wa II mwaka 2002 aliongeza matendo ya mwanga ambapo sasa tunasali tasbihi nne ambazo ni Rozari moja.

Soma zaidi
Mwenyeheri Paulina Marie Jaricot
Ni mwanzilishi wa Uenezaji Imani na Rozari Hai
Bikira Maria mama wa Mungu na Malkia wa Rozari Takatifu
Mt. Filomena
Msimamizi wa Rozari Hai Ulimwenguni na Watoto wote wa Maria

Malengo ya Rozari Hai

Malengo ya Rozari Hai ni kama yafuatayo:

  • Kutuliza hasira ya Mungu aliyekasirishwa na dhambi zetu nyingi mno.
  • Tunamtuliza kwa njia ya maombi ya Mama Maria.
  • Kulinda na kufufua Imani katika roho za Wakristo, na kuwaongoa wakosefu.
  • Kadhalika tunaongeza utukufu wa Mama Kanisa.
  • Kuleta ushindi wa Moyo safi wa Maria. Ushindi ambao aliutabiri Maria katika matukio ya Fatima: “Moyo wangu safi mwishowe utashinda!”
  • Kwa kumheshimu Mt.Filomena aliye somo na mlinzi wa Rozari Hai.
  • Kwa kuwaombea Maaskofu, Mapadri, Watawa, Wagonjwa na Wanaokufa leo ili wapate kifo chema. Kadhalika kwa kuomba Amani katika familia zetu.
  • Kumfanya shetani asiweze tena kuwa na nguvu saa ya kufa kwetu.

Wajibu wa Mwanachama.

  • Mwanachama anapaswa kusali kila siku kumi lake na kutafakari wakati huo fumbo la Rozari linalohusika na kumi hilo. Bila ushirikiano wako. Rozari Haiwezi kuwa hai na hivyo kupoteza thamani yake.
  • Kila mwanachama anashauriwa kufanya saa takatifu mbele ya Yesu. Ekaristi kwa muda wa nusu saa, na/au afanye njia ya msalaba kwa kuwaombea wanachama wa Rozari waliofariki.
  • Kila mwezi Mei kila mwanachama ajitahidi kumheshimu Bikira Maria kwa kufanya ibada zake. Ni vizuri kila mwanachama asali Rozari nzima kila jumapili ya kwanza ya mwezi wa kumi (Oktoba) , ambayo ni sikukuu ya  ROZARI TAKATIFU.
  • Kila mwanachama ajitahidi kuwasaidia wagonjwa na kuona kuwa wanapata sakramenti, pia awashauri na kuwasaidia katika mahitaji yao ya kawaida.
  • Kila mwanachama ajitahidi kuwaombea wagonjwa na wale wanaofariki.

Mawasiliano

  • S.L.P. 90592
    Dar es Salaam
    Tanzania
    East Africa
  • +255 717 558 222
    +255 754 058 801
  • info@rozarihai.or.tz

Ungana nasi

© 2022 Rozari hai. Haki zote zimehifadhiwa. .